Ads 468x60px

Blogroll

Blogger news

About

Thursday, 30 April 2015

SOMO: MACHUKIZO NDANI YA NYUMBA YA MUNGU

SOMO: MACHUKIZO NDANI YA NYUMBA YA MUNGU

(YEREMIA 32:33-34)

“Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa naliwafundisha, nikiondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho. Bali waliweka machukizo yao ndani ya nyumba iliyoitwa kwa jina langu, ili kuinajisi”.

Machukizo ya aina yoyote hayaruhusiwi ndani ya nyumba ya Mungu na ndani ya nyumba zetu.

( KUMBUKUMBU LA TORATI 7:26 )

“na machukizo usitie ndani ya nyumba yako, usije wewe kuwa kitu cha haramu mfano wake; ukichukie kabisa, na kukikataa kabisa; kwa kuwa ni kitu kilichoharamishwa”.

Machukizo yanatajwa kuwa ni kitu kilichoharimishwa. Neno machukizo linatokana na neno la lugha ya kiebrania linaloitwa” toebah”. Neno “TOEBAH” lina maana ya kitu au mtu ambaye ni wa tofauti katika hali. Mtu ambaye ni hatari ukilinganisha na watu wengine. Yatakuwa ni mambo au tabia ambazo ziko kinyume na asili yake.

Machukizo sasa ni vitu vya kipagani ambavyo vimeingia ndani ya nyumba ya Mungu. Yapo mambo ambayo ni machukizo ndani ya nyumba ya Mungu. Mambo ambayo ni haramu kuingizwa ndani ya nyumba ya Mungu.

( i ). Mwanamke kuvaa mavazi ya wanume na mwanamume kuvaa mavazi ya wanawake.

( KUMBUKUMBU LA TORATI 22:5 ). ‘ Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako”.

Mungu anasema maumbile yetu ndiyo yatufundisheni vazi lipi linafaa kuvaliwa na wanaume na ni nlipi linafaa kuvaliwa na wanawake ( 1 WAKORINTHO 11:14 ). Mitindo ya ushonaji nguo iadizainiwa kutokana na maumbile yetu. Ndiyo maana wanawake wana mavazi yao na wanaume wana mavazi yao na Mungu ameliweke hilo mwenyewe. Kwa hiyo vazi kama suruali siyo la mwanamke, limedizainiwa kwa ajili ya mwanamume na si vinginevyo. Katika biblia ni wanaume pekee wanaotajwa wakiwa wamevaa suruali, hatuoni sehemu yoyote ikimtaja mwanamke akiwa amevaa suruali.

Ingia katika blog yangu ujifunze somo la “MAVAZI YA KIKAHABA” utajifunza mengi kuhusiana na mavazi. WWW.davidcarol719.wordpress.com


Suruali kwa wanawake ni vazi la kikahaba kabisa ( MITHALI 7:10 )

( ii ). Sadaka ya kahaba na Mbwa ni machukizo mbele za Mungu

( KUMBUKUMBU LA TORATI 23:18 )

“Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya BWANA, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwaBWANA, Mungu wako yote mawili”. Mbwa ni mtu anayerawiti au mtu anayerawitiwa. Mshahara wa kahaba na watu wote wanaoshiriki katika uchafu wa kurawiti na kurawitiwa ni machukizo kwa BWANA, Mungu wetu. Hatutakiwi kupokea sadaka zao kwa ajili ya BWANA, ni machukizo kwake.

( iii ). Miungu na chochote kinachohusiana na miungu ni machukizo mbele za Mungu.

( EZEKIELI 8:1-18 )

Namna yoyote ya sanamu tunapoihusisha katika ibada tayari inakuwa ni ibada ya miungu. Mapambo ya aina yoyote ni chukizo mbele za Mungu wetu kwa sababu kuna uhusiano kati ya mapambo na miungu. Ni muhimu kufahamu kuwa mapambo hayakuvaliwa na Waisraeli. ( WAAMUZI 8:24 ) “ Kisha Gideoni akawaambia, Mimi nina haja yangu kwenu, ni yakila mtu kunipa hizo pete za masikio ya mateka yake. ( Kwa maana walikuwa na pete za masikio za dhahabu, kwa sababu walikuwa ni Waishmaeli )”. Waishmaeli walikuwa ni wapagani ( mataifa ) vilele waliitwa Wamidiani.

( MWANZO 35:1-4 ).

“……………Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake na wote waliokuwa pamoja naye, Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu,………..Nao wakampa Yakobo, miungu migeni yote iliyokuwa masikioni mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao…………….”.

Mwanamke Yezebeli alikuwa mataifa tena mwabudu miungu. Mwanamke huyo alikuwa staid sana kwa kujipamba na aliingia katika Taifa la Israeli baada ya kuolewa na mfalmeAhabu. Kwa hiyo mapambo yalikuwa yakivaliwa na Waisraeli kwa kuiga tabia za mataifa

( 2 WAFALME 9:30-37; UFUNUO 2:20 )

Makanisa mengi leo yanahudu mafundisho ya Yezebeli ya kuruhusu mapambo kwa watu wa Mungu. Mungu aliwatumia mitume kwa ishara na miujiza mikubwa kutokana na injili yao kuwa kinyume na machukizo. Kanisa la kwanza walifundishwa kuwa mbali na mapambo ya kila namna ( 1 TIMOTHEO 2:9-10; 1PETRO 3:3-5 ).

Kinyume na asili ya Mungu ndiyo maana ya machukizo ( un contrallel to his nature ). Machukizo kwa asili yalikuwa ni ya mataifa na hayakuwa ya Waisraeli.

( YEREMIA 4:1 )

“Kama ukitaka kurudi, Ee Israeli, asema BWANA, utanirudia mimi; na kama ukitaka kuyaondoa machukizo yako, yasiwe mbele ya macho yangu, ndipo hutaondolewa”.

Kuna uwezekano mkubwa hata wakuu wa makuhani ( maaskofu ) kuruhusu machukizo kuingia nyumbani mwa Mungu. Machukizo yakiingia madhara yake ni makubwa kwa watu wa Mungu. Tunaona katika andiko hilo chini kuwa hata uwezo au mkono wa Mungu wa kuponya unaondoka kwa w

( 2 NYAKATI 36:14-16 ).

“Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya BWANA aliyoitakasa katika Yerusalemu. Naye BWANA, Mungu wa baba zao akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake; Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya”.



Miujiza ya Mungu ya uponyaji kama wakati wa Yesu na wakati wa mitume haiwezi kuonekana dhahiri kwa watu wanaoruhusu machukizo kwa watu wa Mungu na ndani maskan i(nyumbani) yake Mungu, Utakuta watu wanashughulika na mapepo tu kila siku lakini miujiza ya vipofu kuona, viziwi kusikia, viwete kutembea, mabubu kuongea, wenye kigugumizi kuongea sawasawa, wenye makengeza kuponywa na kila namna ya miujiza mingine kama nyakati za mitume havionekani. Mamlaka waliyokuwa nayo mitue ya kumwambia kuwete ‘ Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende ( MATENDO 3;6 )’. Mamlaka haiko leo kwa watumishi wengi sababu ni kwamba wameruhusu machukizo nab ado tu wanaendelea kuyatetea kwa bidii nyingi.

( YOHANA 2:13-17 )

Yesu Kristo alipokuta watu wamegeuza hekalu soko alichukizwa mno na kitendo kile ndipo akaamua kupundua meza zao, na kuwaondoa wote hekaluni kwa kutumia kikoto. Aliuliza, Yesu hakuyavumilia machukizo nyumbani mwa baba yake.

Watumishi wa Mungu leo wanatakiwa kufuata msingi aliouweka BWANA YESU na si kuyaacha machukizo eti kwa visingizio vya kulinda kundilisipungue, hatuwasaidii washirika wetu. Tunapaswa kumwondoa mwovu miongoni mwetu ili wengine wajifunze kukaa katika viwango vyote vya neno la Mungu.

( iv ). Wanawake wanapaswa kufunika kichwa wakiwa katika ibada. Wanapaswa kufunika wakiwa kanisani, wanapofanya huduma yoyote ya kiroho mfano, kuomba, kuhutubu au kuhubiri.

( 1 WAKORITHO 11:4-5,7,10,13

‘ Sheria inayomkataza mwanamume kumwomba Mungu akiwa amevaa kofia pia inayomkataza kuvaa kofia kanisani hiyo hiyo ndiyo inayomtaka mwanamke afunike kichwa kwa ajili ya Malaika. Wanaosema ilikuwa desturi za Wakorintho hawayaelewi maandiko vizuri. Biblia inasema ‘ Imempasa mwamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani kwa ajili ya Malaika”. Angalia vizuri neno ‘ imempasa=lazima”. Hakuna Biblia ya Wakorintho pekee yao, tukichambua Biblia hivyo sisi Watanzania hatutabaki na kitabu chichote.Yote yaliyoandikwa, yaliandikwa kwa ajili yetu wote ( WARUMI 2;16 ), Mungu atayahukumu mataifa yote kwa injili hiyohiyo

Tukitaka kuziona nguvu za Mungu waziwazi lazima tuwe mbali na machukizo ya aina yoyote. Mafuta ya Mungu yanakuwa juu ya mtu anayechukia machukizo ( WAEBRANIA 1:9 ). Mtu ambaye anatetea machukizo yaliyomo ndani ya maskani ya Mungu lakini akifanya miujiza au maajabu lazima tujiulize ni nguvu ipi inatenda kazi hapo?. Mungu mwenyewe anasema kuwa mahali penye machukizo, ukono wake wa kuponya hauwezi kuwepo ( 2 NYAKATI 36:14-16 ), Pia hawezi kupakwa mafutaNA Mungu ( WAEBRANIA 1:9 ).

Nyakati hizi tulizonazo watu wengi hawapendi kuambiwa ukweli, wanapenda kudanganywa. Paulo mtume alitabiri juu ya nyakati hizi jinsi watu watakavyotafuta waliu wa kuwafundisha uongo na kuikataa kweli ya neno la Mungu ( 2 timotheo 4:3-4). Hata wakati wa nabii Isaya walikuwepo watu waliotafuta walimu wengine wa mbali na Isaya aliyehubiri kweli yote. Walisema kuwa wanataka mafundisho laini yadanganyayo ( ISAYA 30;9-10 ).Kama tunataka kuishi na Mungu milele hatuna budi kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha na kuwa tayari kuyafuata maagizo yote ya Neno la Mungu ( ZABIRI 119:6 ). Tunasafisha njia zetu kwa kutii neno la Mungu na siyo walimu wetu wanaotufariji tuendelee kufanya machukizo mbele za Mungu ( ZABURI 119;9 ). Walimu wanaowatia moyo watu ili waendelee kuvaa mapambo na suruali kwa wanawake wote ni wafariji wa kutaabisha ( AYUBU 16:2 ).

Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni? Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14). Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27). Kinyonge ni kipi? Ni yule anayetenda dhambi. Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge! Je, wewe ni mtakatifu? Jibu ni la! Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13; YOHANA 14:6). Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni; “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu. Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi. Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo. Bwana Yesu niwezeshe. Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu. Amen”. Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni. Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!

JINSI YA KUELEWA NENO LA MUNGU

Tunaendelea tena leo, kujifunza Kitabu cha YOHANA katika Biblia zetu. Leo tunatafakari YOHANA 7:17-52. Ingawa kichwa cha somo letu la leo ni, “JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU“, kuna mengi zaidi ya kujifunza katika mistari hii. Tutayagawa mafundisho yote tunayoyapata katika mistari hii, katika vipengele kumi:-



(1) JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU (MST. 17);

(2) JINSI YA KUMTAMBUA NABII WA KWELI (MST. 18);

(3) KUSHINDWA KWA WANADAMU WOTE KUISHIKA TORATI (MST. 19);

(4) SABABU KUU YA KUMWITA MTUMISHI WA MUNGU KWAMBA ANA PEPO (MST. 19-20);

(5) WAJIBU NA JINSI YA KUHUKUMU (MST. 21-24);

(6) SABABU KUU YA WATU WENGI KUSHINDWA KUMPENDA MUNGU (MST. 25-29);

(7) SAA YA KUKAMATWA (MST. 30);

(8) NAMI NILIPO NINYI HAMWEZI KUJA (MST. 33-36);

(9) MITO YA MAJI YALIYO HAI (MST. 37-44);

(10) KOSA LA KUMHUKUMU MTU KABLA YA KUMSIKIA (MST. 31-32, 45-

52).


(1) JINSI YA KULIELEWA NENO (MST. 17)

Biblia, ni kitabu kinachochapishwa na kutolewa nakala nyingi sana na kusambazwa na kusomwa kwa wingi, kuliko Kitabu chochote kile kingine ulimwenguni, katika wakati wote na miaka yote. Kwa mfano, kulingana na vitabu vyenye takwimu, “ENCYCLOPAEDIA BRITANNICA“ na “ENCYCLOPAEDIA AMERICAN“, mwaka 1932 peke yake Biblia zilizoschapishwa na kusambazwa kwa lugha mbalimbali duniani, zilikuwa 1,330,213,815. Miaka 50 iliyopita kulingana na mtafiti anayeitwa HY PICKERING, ili kukidhi mahitaji ya Biblia, Chama cha Biblia cha BRITISH AND FOREIGN BIBLE SOCIETY, kililazimika kuchapa nakala moja ya Biblia kila baada ya SEKUNDE TATU mchana na usiku au karibu nakala 32,876 kila siku katika mwaka mzima. Biblia hizi zilisambazwa katika ulimwengu mzima kwa kutumia makasha 4,583 yenye uzito wa karibu TANI 500! Hata hivyo, jambo la kushangaza ni kwamba mamilioni ya watu wanaosoma Biblia hawaielewi! Tunajuaje kwamba hawaielewi? Maisha ya watu hawa hayabadiliki na kufuata maelekezo ya Neno la Mungu. Tatizo ni nini? Jibu tunalipata katika MST. 17 “MTU AKIPENDA KUYATENDA MAPENZI YAKE (MUNGU), ATAJUA HABARI YA YALE MAFUNZO“. Kama mtu hayuko tayari kulitenda kila jambo atakalofundishwa na Mungu katika Neno lake, Roho Mtakatifu humwacha mtu huyo, hawezi kumfunulia chochote katika Neno la Mungu. Matokeo yake hawezi kuelewa lolote! Bila roho Mtakatifu hatuwezi kufunuliwa na kulielewa Neno la Mungu (1 WAKORINTHO 2:10, 13; YOHANA 16:13). Wengi wetu hatulielewi Neno kwa sababu hatuko tayari kulitendas. Hatua yoyote ya kushindana na kupingana na Neno la Mungu, humfanya Roho Mtakatifu kutuacha mara moja. Kabla ya kulisoma neno au kujifunza Neno la Mungu kwa njia yoyote, ili tulielewe Neno la Mungu, hatuna budi kuwa na msimamo wa kutaka kulitenda Neno lake sawasawa na (YEREMIA 42:1-6).



(2) JINSI YA KUMTAMBUA NABII WA KWELI (MST. 18)

Yeye anenaye kwa nafsi yake tu, huyo siyo nabii wa kweli. Kunena kwa nafsi yake mtu, ni kuhubiri au kufundisha kinyume na Neno la Mungu. Mtu wa jinsi hii, hatafuti Utukufu wa Mungu, bali wake mwenyewe. Nabii wa kweli humhubiri Kristo, au kwa jinsi nyingine, hulihubiri Neno! (WAFILIPI 1:18; 2 TIMOTHEO 4:2).



(3) KUSHINDWA KWA WANADAMU WOTE KUISHIKA TORATI (MST. 19)

Wanadamu wote mble za macho ya Mungu, hakuna hata mmoja aliyeweza kuishika torati, maana mtu akiishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, anahesabiwa kukosa juu ya yote (YAKOBO 2:10). Hivyo, mbele za Mungu, hakuna mwanadamu atendaye mema, la, hata MMOJA! (WARUMI 3:10, 12; 1 YOHANA 1:8). Wanadamu wote tulistahili kuangikwa msalabani kama adhabu ya laana ya kutokuishika torati (WAGALATIA 3:10; KUMBUKUMBU 21:22-23). Aliyempendeza Mungu sikuzote, na kufanya yaliyompendeza, ni Yesu Kristo pekee (MATHAYO 3:17; YOHANA 8:29). Ni kwa sababu hii, tunahesabiwa haki BURE kwa neema yake, kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu kwa imani katika damu yake iliyomwagika msalabani, alipokufa kwa niaba yetu, ili awe upatanisho (WARUMI 3:24-26; 1 TIMOTHEO 2:5-6).



(4) SABABU KUU YA KUMWITA MTUMISHI WA MUNGU KWAMBA ANA PEPO (MST.19-

20)

Mtumishi yeyote wa Mungu anayeyafichua maovu yaliyo……………………………. katika jamii ya watu wanaojiita Wakristo, na kuyanena waziwazi kwamba hayampendezi Mungu, na kuisema kweli, huyu sharti watu hao watamwita ana pepo. Dhambi zinapokubalika katika Kanisa lote la Mungu na watu wanaojiita Wakristo, wanapokuwa hawana tofauti na wapagani au mataifa, anapoinuliwa Mtumishi wa Mungu na kuleta mageuzi, sharti mtu huyo ataitwa ana pepo. Yesu hapa alifichua maovu yao na kuisema kweli kwamba wanataka kumuua, wao wakakana, wakaipinga kweli hiyo wakati ilikuwa kweli; kinyume chake wakamwita ANA PEPO, ili kujikosa na kuhalalisha maovu yao! (MST. 19-20, 23). Hivyo ndivyo inavyokuwa wakati awote. Haya yalimpata Martin Luther, John Wesley, Charles Finney na wote walioleta mageuzi ya jinsi hii nyakati zao.



(5) WAJIBU NA JINSI YA KUHUKUMU (MST. 21-24)

“Ifanyeni hukumu iliyo haki“, ni mafundisho ya Yesu Kristo kwetu. Hatupaswi kukaa kimya kwa visingizio vya Neno, “Msihukumu“, na kuacha kuyakosoa mafundisho potofu ya Mashahidi wa Yehova; Mormonism au Christ Church for Latter Day Saints, wanaoshika mafundisho ya Joseph Smith; au wanaojiita Wakristo na kusema wao siyo dhehebu, wanaofuata mafundisho ya William Branham; au mafundisho yanayofundisha watu kushika sabato leo, au mafundisho mengine yoyote yaliyo potofu. Kukaa kwetu kimya na kuogopa “kuyasema madhehebu mengine“, siyo kufuata nyayo za Mchungaji Mkuu wa Kondoo, Yesu Kristo na kufanya hivyo, ni kuwaachia kondoo wetu wararuliwe na mbwa mwitu. Huo ni uchungaji wa mshahara. Yesu aliifanya hukumu iliyo haki, pale alipokuwa kinyume na kuishika Sabato, na tena pale aliposema “Jilindeni na *chachu* au mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo“. (MATHAYO 16:11-12; YOHANA 10:12; MATENDO 20:28-30). Tunapaswa kufuata kielelezo cha Yesu. Kanisa la Kwanza walizingatia kufanya hivyo (WARUMI 16:17; 2 YOHANA 1:9-11). Watu wenye mafundisho potofu, hatupaswi kuwa na ushirika nao, tuwahesabu tu kama mataifa na kuwahubiria kweli na kutokukubali kusikia chochote kutoka kwao.



(1) SABABU KUU YA WATU WENGI KUSHINDWA KUMPENDEZA MUNGU

(MST.25-29)

Tangu zamani za kale, sababu kuu ya watu wengi kushindwa kumpendeza Mungu, ni watu hao kuacha kumwamini Yesu na kuokolewa, kwa kungoja kwanza WAKUU WAMWAMINI (MST. 26). Wengine wanangoja kwanza baba na mama, mume au kiongozi wao wa dini aokoke, ndiyo eti nao waokoke, na wanafuata mafundisho yao tu kimkumbo. Huu ni mtego mkubwa wa Ibilisi. Ukitengwa ugali mezani kila mtu huchukua tonge lake mwenyewe! Ndivyo ilivyo, damu imemwagika msalabani, wokovu tayari. Kila mmoja anapaswa kuuchukua kwa imani. Ni muhimu kukumbuka pia kwamba, kila mtu atalichukua furshi lake mwenyewe na kutoa habari zake MWENYEWE (WARUMI14:12; WAGALATIA 6:5). Hakuna haja ya kungoja wakuu waokoke ndiyo nasi tuokoke. Kufa hakufuati nani wa kwanza kuzaliwa!.



(7) SAA YA KUKAMATWA (MST. 20).

Maadui zetu watatutafuta sana ili watushike na kutudhuru, hata hivyo, hatupaswi kuhofu. Hatuwezi kufa mpaka saa yetu itakapowadia. Juhudi zao zitagonga mwamba, wakati wote Bwana wetu atatupa mlango wa kutokea maana amesema atakuwa pamoja nasi hat ukamilifu wa dahari yaani mwisho wa mambo yote (MATHAYO 28:19-20; AYUBU 5:20, 26-27).



(8) NAMI NILIPO NINYI HAMWEZI KUJA (MST. 33-36)

Hatuwezi kumwona Yesu pasipo Utakatifu na kutafuta kwa bidii kuwa na amani na watu wote (WAEBRANIA 12:14). Ni wale tu wenye mioyo safi watakaomwona Mungu (MATHAYO 5:8). Ikiwa tumejaa masengenyo, chuki, fitina, hasira, mawazo machafu, n.k. tutamtafuta Yesu tusimwone.

(9) MITO YA MAJI YALIYO HAI (MST. 37-44)

Mtu akimpokea Roho Mtakatifu, ishara ya kwanza itakayoonekana kwake, ni kunena kwa lugha mpya kadri roho atakavyomjalia kutamka (MATENDO 2:4; 10:44-46; 19:6). Maji yanapokuwa yanapita katika mto, hutoa aina fulani ya sauti isiyoweza kuelezeka. Ndivyo alivyo mtu anenaye kwa lugha baada ya kumpokea Roho, mito ya maji hutoka ndani yake!



(1) KOSA LA KUMHUKUMU MTU KABLA YA KUMSIKIA KWANZA NA KUJUA

ATENDAVYO (MST. 31-32, 45-52)

Watu wengi hufanya kosa la kumhukumu Mtumishi wa Mungu kabla ya kumsikia kwanza anenavyo au anavyofundisha na kujua atendavyo. Haitupasi kufanya hivi. Watumishi waliotumwa na makuhani kumkamata Yesu, walikubali kwanza kumsikia na wakagundua kweli waliyokuwa wamefichwa na Shetani. Kuna faida kubwa kuiga mfano wao.

…………………………………………………………………………………………………………………………………. .

Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni? Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14). Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27). Kinyonge ni kipi? Ni yule anayetenda dhambi. Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge! Je, wewe ni mtakatifu? Jibu ni la! Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13; YOHANA 14:6). Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni; “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu. Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi. Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo. Bwana Yesu niwezeshe. Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu. Amen”. Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni. Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!

NGUVU NYUMA YA JINA LAKO.



NGUVU NYUMA YA JINA LAKO.


BAADHI YA WATU WALIOBADILISHWA MAJINA KATIKA BIBILIA:
THE POWER BEHIND YOUR NAME

Haya ni baadhi tu ya majina na maana zake kwa ufupi.
 
1. Abramu – Ibrahamu – Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Tafsiri ya jina Abramu ilikuwa ni MUUMBAJI WA NAFSI (a souls creator
; High father), maana ambayo Ilikuwa na uhusiano na mambo ya kishirikina. Ni kama wale wataalam wa kiganga. Alibadilishwa kwenda Ibrahimu – Baba wa mataifa.
2. SARAI –SARA- Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Jina Sarai - lilimaanisha Binti wa kifalme. Tatizo lilikuwa ni binti wa Kifalme, katika ufalme upi. Ndiyo maana Mungu akaamua kufanya badiliko dogo katiaka jina lake.
• Jina Sara - linamaanisha Mwanamke aliye katika ngazi ya juu, mama wa mataifa mengi.
• Mungu alimbadilisha Sarai jina ili kuonesha hatua ya badiliko kutoka katika hatua ya chini kwenda hatua ya juu na kumfanya kuwa mama wa mataifa. (The name-change indicates a step from local to global)
3. Yakobo - Israeli - Alibadilishwa na Mungu mwenyewe.

• Jina Yakobo/James – lilimaanisha mtu mdanganyifu, mwenye hila
• Jina Israeli - linamaanisha taifa la Mungu.
4. Simoni mwana wa Yohana – Petro– Alibadilishwa na Yesu.
• Jina Simoni – lilimaanisha ………………………….
Jina Petro – lilimaanisha jiwe/ mwamba

5. Sauli – Paulo – Alibadilishwa na Yesu
• Sauli ilimaanisha mtu wa maangamizi/kifo (Angalia Sauli wa Agano la Kale alitafuta kumuangamiza Daudi. Aliangamiza watu wengi sana katika utawala wake. Sauli wa Agano Jipya naye alitafuta na kuangamiza wakristo wengi sana mpaka pale alipookolewa.

• Paulo ilimaanisha mtu mdogo aliyejishusha.

6. Daniel - Belteshaza - Alibadlishwa na mkuu wa matowashi wa mfamle Nebukadreza
danieli na wenzake walipofika tu uhamishoni, kitu cha kwanza kilikuwa ni kubadilishwa majina yao.
Jina Danieli – lilimaanisha mtumwa w…..

Watu wengine waliobadilishwa majina yao kwenye maandiko utajisomea mwenyewe kwenye kitabu hiki NGUVU NYUMA YA JINA LAKO


12. Agness Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “ safi, takatifu”.
13. Adamson – Asili ya Kiingereza ya zamani, na maana yake ni “mwana wa Adamu”.
14. Aden- Asili ya Kig
iliki, na maana yake ni “moto”.
15. Aisha – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “ yu hai na mwenye afya njema”.
16. Aaliya – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “mwenye asili ya kifahari”.
17. Amina – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “aliyemkweli na mwaminifu”.
18. Anisa – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “neema au upendeleo/kibali”.
19. Michael – ni nani aliye kama Mungu.
20. Amani – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “ hamu; matarajio au matakwa”.
21. Samson – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “Jua”.
22. Nicholas – Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “watu wa ushindi”.
23. Margaret – Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “Lulu mwanamke wa thamani”.
24. Ester – Asili ya Kiajemi, na maana yake ni “Mtu mwororo, jani la mti mwororo,”.
25. Faraja – Asili ya Kiswahili, na maana yake ni “faraja, nafuu au pumziko”.
26. Editha, Edith – Asili ya Kiingereza, na maana yake ni “Mwanamke wa mashindano kwa ajili ya mali”.
27. Jane – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “neema ya Mungu”.
28. Halima – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “mpole, mwenye tabia ya kati.”
29. Linda – Asili ya Kihispania, na maana yake ni “mzuri wa sura”.
30. Flora – Asili ya Kilatini, na maana yake ni “Ua”.
31. Victoria/Victor - Asili ya Kilatini, na maana yake ni “ushindi”.
32. Jessica – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “Anayeona”.


33. Emma – Asili ya Kifaransa na Kijerumani ya zamani, na maana yake ni “yote, ya kiulimwengu

 
Blogger Templates